WOKOVU - KAZI KUU YA MUNGU
- 6 -
Wokovu ni Nini?
Katika mwanzo wa kitabu hiki tulieleza wokovu ni kurejezwa au kupatanishwa katika uhusiano wetu na Mungu. Sasa tufafanue zaidi maana yetu tukiunganisha yale tuliyojifunza hadi sasa:
Wokovu ni kazi ya Mungu kumwokoa mwenye dhambi kutoka katika utawala wa Shetani na adhabu ya dhambi na kutengeneza uhusiano na ushirikiano kati ya mwenye dhambi na Mungu na kumweka chini ya utawala wa Mungu.
Kwa ufafanuzi zaidi wokovu ni kuokolewa kutoka hali moja hadi hali nyingine mpya tunayopewa na Mungu.
KUTOKA HADI
Mfu Kiroho Hai Kiroho
Utawala wa Shetani Utawala wa Mungu
Utumwa wa dhambi Utumwa wa Mungu
Utumwa wa Utu wa Kale Kutawala Utu wa Kale
Ghadhabu ya Mungu Upendo wa Mungu
Hukumu ya Mungu Kibali cha Mungu
Laana ya Mungu Baraka ya Mungu
Hali ya Uchafu Hali ya Usafi
Kutenganishwa na Kristo Kuunganishwa na Kristo
Kutokuwa na Tumaini Kuwa na Tumaini
Kuwa mwenye Hatia Kuwa Mwenye Haki
Adui ya Mungu Rafiki ya Mungu
Wokovu ni kazi ya Mungu kumwokoa mwenye dhambi kutoka katika utawala wa Shetani na adhabu ya dhambi na kutengeneza uhusiano na ushirikiano kati ya mwenye dhambi na Mungu na kumweka chini ya utawala wa Mungu.
Kwa ufafanuzi zaidi wokovu ni kuokolewa kutoka hali moja hadi hali nyingine mpya tunayopewa na Mungu.
KUTOKA HADI
Mfu Kiroho Hai Kiroho
Utawala wa Shetani Utawala wa Mungu
Utumwa wa dhambi Utumwa wa Mungu
Utumwa wa Utu wa Kale Kutawala Utu wa Kale
Ghadhabu ya Mungu Upendo wa Mungu
Hukumu ya Mungu Kibali cha Mungu
Laana ya Mungu Baraka ya Mungu
Hali ya Uchafu Hali ya Usafi
Kutenganishwa na Kristo Kuunganishwa na Kristo
Kutokuwa na Tumaini Kuwa na Tumaini
Kuwa mwenye Hatia Kuwa Mwenye Haki
Adui ya Mungu Rafiki ya Mungu
Mchoro #8 – Mtu wa kushoto bado hajaokolewa. Bado yuko chini ya utawala wa Shetani na dhambi. Mtu wa kulia ameokolewa na yuko katika uhusiano mzuri na Mungu.
Tunaona katika mchoro #8 kwamba:
Yaani, wokovu ni kutoka katika hali fulani ili tupewe hali nyingine mpya. Jambo muhimu katika hali mpya ile ni uhusiano wetu na Mungu. Uhusiano wa kuwa chini yake na uhusiano wa kushirikiana naye katika upendo, imani, na ibada. Katika sehemu ya pili ya kitabu hiki tunaangalia zaidi maana ya kuwa katika uhusiano na Mungu.
Tunaona katika mchoro #8 kwamba:
- Wokovu siyo kujitahidi kumpendeza Mungu
- Wokovu siyo kuokoa mtu kutoka utawala wa Shetani na dhambi tu ili ajitawale
- Wokovu siyo kukoa mtu asiadhibiwe tu
Yaani, wokovu ni kutoka katika hali fulani ili tupewe hali nyingine mpya. Jambo muhimu katika hali mpya ile ni uhusiano wetu na Mungu. Uhusiano wa kuwa chini yake na uhusiano wa kushirikiana naye katika upendo, imani, na ibada. Katika sehemu ya pili ya kitabu hiki tunaangalia zaidi maana ya kuwa katika uhusiano na Mungu.